NYOMI KAMPENI ZA DKT. SAMIA KIGOMA MJINI

ccmkwanza
3 Min Read

Sehemu ya wananchi wakiwa katika mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM,Dkt Samia Suluhu Hassan  Kigoma Mjini, Septemba 14, 2025.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan asubuhi hii anahitimisha kampeni zake katika Mkoa wa Kigoma baada ya jana kufanya Uvinza, Kasulu na Buhigwe.

Kama kawaida katika mkutano mkubwa utakaofanyika Kigoma Mjini ataelezea mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha uongozi wake wa miaka minne na kutoa ahadi za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.



Kigoma ni kati ya mikoa michache sana ambayo ina miradi mingi sana ya maendeleo. Ndani ya miaka 4 ya Rais Samia mkoa huo umepokea zaidi ya Sh Trilioni 11 kwenye sekta mbalimbali za maendeleo

‎Baadhi ya miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea na utekelezwaji mkoani Kigoma ni hii ifuatayo,

‎Ujenzi wa Barabara Kuu za lami zaidi ya km 420 zikiwemo za Kibondo-Mabamba na Kibondo-Marongwe

‎Ujenzi wa Barabara za mitaa km 10 chini ya Tactic

‎Ujenzi na Ukarabati wa Bandari ya Lagosa,Kibirizi

‎Ujenzi wa meli Mpya na Chelezo ya Kuundia meli

‎Ukarabati wa meli za mv Sangara na Mv Liemba Ziwa Tanganyika

‎Ujenzi wa Station kuu ya Sgr Kigoma

‎Ujenzi wa SGR Tabora-Kigoma(Main Camp ni Uvinza-Kigoma)

‎Ujenzi wa Soko Kuu la Mwanga na soko la Katonga via Tactic

‎Ujenzi wa Tawi la Chuo Kikuu Cha Muhimbili

‎Ujenzi wa Tawi la Chuo Cha Uhasibu TIA

‎Upanuzi wa Chuo Cha Taifa Cha Hali ya hewa na Ufungaji wa radar

‎Ujenzi wa Hospital ya Rufaa ya Kanda ya Magharibi

‎Ujenzi,ukarabati na upanuzi wa uwanja wa Ndege wa Kigoma (Gombe-Mahare International Airport)

‎Ujenzi wa njia kubwa ya kusafirisha Umeme wa Kv 400 Nyakanazi-Kidahwe

‎Ujenzi wa Tawi la BoT Kanda ya Magharibi (Usanifu unaendelea)

‎Ujenzi wa Katosha Dry Port

‎Ujenzi wa meli mpya ya abiria na mizigo

‎Ujenzi wa meli ya abiria

‎Ujenzi wa Chuo Cha Umahili wa Tehama Buhigwe

‎Miradi kedekede ya maji ya zaidi ya Sh. Bilioni 429

‎Ujenzi wa Malagarasi Hydropower Project

‎*Ujenzi wa kiwanda kipya cha Saruji Cha Tanzania Cement Company ltd

‎*Mradi wa ujenzi wa Kiwanda Cha Pamba na Kiwanda Cha Sukari Kasulu.

featured Siasa

Share This Article
Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *