Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dodoma ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wa mkoa huo, Dkt. Neema Majule ameihoji Serikali bungeni Dodoma Juni 4, 2026, kwamba jinsi gani wanawake na vijana watakavyoshiriki uchumi jumuishi?
Aidha, Dkt. Majule ameihoji tena serikali kwamba itaweka viashiria gani kupata ushiriki wao kwa mitaji nafuu, masoko, technolojia, ajira ili ukuaji wa uchumi huo usibaki kwa wachache?